Ads

ACT WAZALENDO WAICHAMBUA SEKTA YA ELIMU NCHINI

Serikali imetakiwa kutoendelea kujitapa kwa kuweka fedha nyingi katika ujenzi wa madarasa, bali imetakiwa kuhakikisha inaweka mazingira wezeshi ya watoto kujisomea pamoja na maslahi ya walimu ili watoe elimu bora.
Image result for ADO SHAIBU
Hayo yamesemwa mapema leo jijini Dar es salaam na msemaji wa Chama cha ACT Wazalendo Ndugu Addo Shaibu wakati akitoa tathmini ya hali ya elimu hapa nchini.

Ndugu Addo alisema kuwa kiwango cha elimu nchini kimeshuka na kusababisha wanafunzi wengi hasa wa shule ya msingi kutojua kusoma na kuandika, kwani hapo mwanzo darasa moja ililitakiwa kuwa na wanafunzi 48 kwa mwalimu mmoja lakini kwa sasa wanafunzi 52 na zaidi hali inayoonyesha walimu kuelemewa.

Aliendelea kusema kuwa sababu ya walimu kushindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo ni kuwa na malimbikizo mengi ya mishahara yao, kukosa nyumba za kuishi, kukosa nyenzo za kufundishia na n.k hali inayosababisha walimu kushindwa kufanya kazi kwa weledi na hatimaye kuvujisha mitihani ili kupata mahitaji yao muhimu.

Na mwisho kabisa alipenda kuishauri serikali kuweza kutoa takwimu sahihi kuhusiana na hali ya elimu hapa nchini, lakini pia kuwapa ajira walimu wenye vigenzo na kuangalia elimu bora na siyo kuangalia matokeo ya vyeti kwani mtu anaweza kununua na kwenye ufanisi akawa mbovu vilevile.

No comments