Ads

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI ILALA AVIONYA VYAMA VYA SIASA KUTOTUMIA VIONGOZI WA DINI KATIKA KAMPENI.



Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Jumanne Shauri, akizungumza na waandshi wa habari  (hawapo pichani) katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya ilala mapema leo ( Picha na John Luhende)

Na John Luhende 
Mwamba wa habari
Msimamizi wa Uchaguzi  wa  Maispaa ya Ilala ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Jumanne  Shauri , amevitaka vyama vyote vya siasa vinavyo shiriki uchaguzi wa Ubunge jimbo la Ukonga  na udiwani katika kata za Zingiziwa na Vingunguti kufuata sheria na maadili ya  uchaguzi ili kuepuka vurugu zinazoweza kujitokeza.

Msimazi huyo ameyasema hayo leo wakati akizunguza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa kampeni zinazoendelea wilayani Ilala nakusema kuwa kampeni zinaendelea vizuri  japo kuna malalamiko macheche huku akivionya vyama vya siasa kutotumia viongozi wa Dini katika kampeni zao.

‘’kuna suala la kutumia viongozi wa dinini katika kampeni mimi kama msimamizi wa uchaguzi  nasema kama kunachama chochote cha siasa kitakacho tumia viongozi wa dini tutakipa adhabu”amesema.

Aidha ameviasa vyama hivyo kujikita zaidi katika kunadi  Ilani za vyamavyao badala ya kuzumnguza matusi na maneneo ya kibaguzi ili wananchi waweze kuchagua wayoitaka.

Pamoja nahayo  Msimamizi huyo ameeleza namna uchaguzi huo utakavyo endeshwa siku ya kupiga kura,kwamba vituo vya kupigia kura vitafunguliwa saa moja  asubuhi hadi saakumi jioni  na kufuatiwa na zoezi la kuhesabu kura.

No comments