Ads

ZIARA YA DC MJEMA YAMUIBUAMTUHUMIWA WA MBAKAJI SUGU PUGU.






Mwamba wa habari
Na John Luhende
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe Sophia Mjema  ameamuru kukamatwa na kuwekwa ndani  pamoja na kufanyiwa uchunguzi kwa mkazi mmoja wa  Pugu mnadani mara baada  yakulalamikiwa na  baadhi ya wakazi wa eneo hilo  wakimtuhumu kumbaka mtoto wake wakike anayekadiriwa kuwa na miaka saba.


Shutuma hizo zimetolewa na wakazi hao katika mkutano wa DC  Mjema ulifanyika Pugu mnadani kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi wa eneo hilo ikiwa ni siku ya tatu ya ziara yake jimboni ukonga kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia majawabu.

Mkazi mmoja  huyo ambaye jina lake tumelihifadhi anaeleza namna mtoto huyo anavyoishi mazingira magumu kwa sababu ya vitendo vya kikatili anavyo katendewa na Babayake.



Mkazi huyo ameeleza mbele ya DC Mjema , kuwa baada ya kufuatilia alibaini ukweli kuwa mtoto anatendewa vitendo hivyo vya kikatili kila siku jambo ambalo limemfanya mototo huyo kutoroka mara kwa mara .

Msamalia mwema huyo ameendelea kudai kuwa hata majirani wanafahamu kuhusu jambo hilo lakini wamekuwa wakikosa ushirikiano kutoka kwa baba huyo kujua ukweli kuhusu maisha ya mtoto huyo.

Mara baada ya madai hayo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia  Mjema , alimwita mtuhumiwa huyo lakini alikuwa ameshanza kutoroka  mkutanoni hapo na kwenda kubadili mavazi aliyokuwa nayo mwanzo lakini akafuatwa na kukamatwa  huku akijitia mwenda wazimu  akijibu mambo  tofauti na anacho ulizwa.

Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani   pindi uchunguzi wa  kipimo cha  DNA utakapo fanyika  kama alivyo agiza   DC Mjema , na mtoto huyo kwa sasa yuko amepelekwa hospitali hapa jijini Dar es Salaam.

No comments