Ads

ZIJUE FAIDA ZA KUJIUNGA NA BIASHARA CLUB YA KCB BENKI

Biashara Club ni mfumo uliyoundwa mahususi kwa ajili ya kuwakutanisha pamoja wafanyabiashara wanaotumia huduma za kibenki kutoka benki ya KCB kuweza kufahamiana na kubadilishana uzoefu katika mambo ya kibiashara.
 Mkurugenzi Mtendaji wa KCB Benki Bw. Cosmas Kimario akitoa ufafanuzi wa jambo fulani mapema leo jijini Dar es salaam katika mkutano na wadau wa Benki hiyo.

Akiongea na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es salaam baada ya mkutano kati ya benki hiyo na wateja wake Mkurugenzi Mtendaji wa KCB Benki Bw. Cosmas Kimario alisema kuwa club hiyo inafaida kubwa kwa wafanyabiashara kwa kuwa inawakutanisha wafanya biashara wengi wa ndani na nje ya nchi kuweza kukaa pamoja na kujadili mambo ya kibiashara, changamoto na jinsi ya kuzipatia ufumbuzi.

Katika mkutano huo uliofanyika mapema leo julai 25 katika hoteli ya Serena uliwakutanisha zaidi ya wafanyabiashara 250 wa ndani na miongoni mwao wakiwa wafanyabiashara wakubwa wa kati na wafanya biashara wadogo waliopo katika club hiyo ya KCB Biashara.

Mkurugenzi huyo aliongezea kuwa benki ya KCB inawapa fursa mbalimbali wafanyabiashara hao kwa kuweza kutembelea nchi mbalimbali ili kuweza kujifunza mambo mengi zaidi kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa na kuweza kufanya biashara nao ili kupanua wigo wa biashara zao, ikiwa kwa mwaka jana walitembelea nchi ya China na kwa mwaka huu walipata nafasi ya kwenda nchini Japani.

“Lakini pia ziara hizi zimekuwa na manufaa makubwa kwa wafanya biashara kuweza kukutana na watu wanaofanya nao biashara kwa kutumia njia ya simu na mtandao lakini hapa wataweza kuonana nao Mubashara na kujadili vitu vingi kuhusu biashara, ikiwa kupata mapunguzo ya bei za bidhaa endapo wataagiza na pia wanatengeneza uaminifu na wafanya biashara hao” alisema Mkurugenzi
Mshauri wa Masuala ya biashara Bw. Adolf Lymo akiongea na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es salaam katika mkutano ulioandaliwa na Benki ya KCB.

Kwa upande wake Mshauri wa mambo ya kodi kwa wafanyabiashara Bw. Adolf Lymo alisema kuwa kwa leo amekuja kutoa elimu ya ulipaji kodi na faida zake, kwa wafanyabiashara wakubwa wadogo na hata wakati ili wajue kulipa kodi ndio msingi wa maendeleo kwa taifa lolote duniani.

"Changamoto kubwa wanayokutana nayo wafanyabiashara wengi ni kupuuzia na kutozingatia ulipaji wa kodi na kujisahau kuwa unapokuwa na biashara yeyote basi ujue kuwa serikali nayo inakuwa ni mbia kwenye biashara hiyo kwa kutegemea kuendesha vema maendeleo yake kupitia kodi yako".Alisema Adolf 



Baadhi ya wafanyabiashara wakifuatilia mkutano kwa makini

No comments