WADAU WA JUKWAA LA KILIMO WAZUNGUMZIA UMUHIMU WA KUONGEZEWA KWA MAAFISA UGANI KATIKA HALMASHAURI NCHINI.
| Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Mtendaji wa Jukwaa la wadau wa Kilimo, (ANSAF)Audax Rukonge akizungumza na Waandishi wa habari hawapo picha ni wakati wa MKutano wa wadau wa Killimo kujadilia masuala mbali mbali kuhusu Kilimo. |
Mwambawahabari
Serikali imeshauriwa kusambaza Maafisa Ugani kwenye Halmashauri mbali mbali nchini ili waweza kumsaidia Mkulima aweze kufanya Kilimo kwa Ufanisi na kuongeza mavuno.
Serikali imeshauriwa kusambaza Maafisa Ugani kwenye Halmashauri mbali mbali nchini ili waweza kumsaidia Mkulima aweze kufanya Kilimo kwa Ufanisi na kuongeza mavuno.
Ushauri huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Mtendaji wa Jukwaa la wadau wa Kilimo (ANSAF),Audax Rukonge wakati wa Mkutano uliowashirikisha wadau mbali mbali wa Kilimo kujadili kuhusu huduma za Ugani kwa kulima ili ziendane na shughuli ya Viwanda hapa nchini.
Amesema kitendo cha sasa cha kumtumia Afisa Mgani mmoja katika Kijiji kimoja ni kitendo ambacho hakiwezekani katika kumsaidia Mkulima.
“Afisa Ugani katika Kijini Kimoja, ni kitu hakiwezekani,maana leo tunasema tuna kijiji kimoja na kesho tukawa na vijiji ishirini hivyo itashindikana kwa afisa Ugani huyu kufanya kazi kwenye vijiji vyote, ni vema serikali ikaliangalia hili”Amesema Rukonge.
Amesema kutokana na hali ilivyo ya uchache wa Maafisa Ugani kunahaja ya sekta binafsi kuwekeza kwenye utoaji wa Huduma ya Ugani kwa Wakulima ili iwe rahisi kwa Mkulima kusaidika.
“Sasa kuna haja sekta binafsi kuwekeza kwenye kutoa huduma ya Ugani kwa wakulima ili waweze kulipia kwa kiasi husika cha fedha ,kwa mfano kwa wale wakulima wafugaji kama Ngome anaumwa Nyumbani hanahaja ya kumsubili aje Afisa Ugani bali anamtafuta Afisa ugani wa Sekta Binafsi anampa hela anamsadia “Amesema Rukonge.
Kwa Upande wake Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokine (SUA)Dk Sizya Lugeye ambaye ni miongoni wa wadau hao katika mkutano huo, ameishauri serikali Kuhakikisha wanawaongezea nguvu maafisa Ugani waliopo ikiwemo kuwapata fedha pamoja vitendea kazi ili waweze kufanya kazi kwa ufanizi zaidi katika kuwahudumia wakulima.

Post a Comment