Ads

TAARIFA YA MEYA WA JIJI LA DAR ISAYA MWITA AKIKANUSHA KUHUSU KUDAIWA KUTAKA KUHAMA CHAMA CHA CHADEMA

Ndugu

waandishi wa habari: Nimeshikwa na mshtuko, simanzi baada ya kusambaa 
kwa  taarifa ambazo naweza kusema kuwa ni za uzushi kwamba  
ninampango wa kujiondoa ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo 
Chadema. naomba taarifa hizo zipuuzwe manahazina ukweli wowote na kwamba
zinampango wa kunichafua mimi pamoja na Chama Changu.


Ndugu 
wandishi wa habari : Napenda ieleweke kuwa  sijawahi kudhani wala 
kufikiria kuhama Chadema na kwenda kwenye chama chochote kile cha siasa.
Chadema ni chama ambacho nimetoka nacho mbali tangu mwaka 2004 hadi 
leo, nimejenga chama kwa gaharama zangu mwenyewe.

Ndugu waandishi
wa habari: Leo nimekuwa Meya wa jiji la Dar es Salaam kupitia Chama 
Changu cha Chadema,natambua kuwa  chama kimeniheshimu sana kwa kunipa 
nafasi hii hivyo sina sababu ya kuondoka kwani  ninania ya kuwatumikia 
Wananchi ambao wameniamini na wamenichagua kwa mapenzi yao wakiamini 
kuwa nitawaletea Maendeleo nikiwa ndani ya Chama Cha Chadema.

.Nafahamu 
tuhuma hizi zinatokana na aina ya utendaji wangu katika Jiji la Dar es 
Salaam kwani nimekuwa nikifanya kazi badala ya kupambana na serikali 
pale ambapo watu wanaamini kuwa mambo hayajaenda sawa.

Ndugu 
waandishi wa habari:  Kukaa kwangu kimya huku ,kutokufanya siasa za 
kiharakati ndani ya jiji la Dar es Salaam  haimanishi kwamba nipo upande
wowote ama kukihujumu chama changu. Ila huu ni mfumo ambao nimeuchagua 
na kujijengea kwa ajili ya kuwatumikia wananchi nasio kufanya harakati 
za kisiasa kwakuwa nina  nia  ya kufanya maendeleo ndani ya jiji la Dar 
es Salaam.

No comments