WADAU WA KILIMO NDANI NA NJE YA NCHI KUKUTANA SIKU TATU KUJADILI MCHANGO WA KILIMO KATIKA TANZANIA YA VYA WANDA
Ba John Luhende
mwambawahabari
mwambawahabari
Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Tatu wadau wa Sera za Kilimo AAPC utakafanyika kesho jijini Dae es salaam ambapo Waziri wa Kilimo , Mifugo na Uvuvi Mhe. Charles Tzeba atakuwa mgenirasm, atakaye zindua taarifa ya Bank ya Dunia kuhusu hali ya mazingira wezeshi ya biashara Tanzania .
Akizunguza na waandishi wa Habari Mkurugenzi mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na Kilimo ANSAF Bwana Audax Lukonge amesema mkutano huo pamoja na Mada mbalimbali zitakazojadiliwa pia watatazama Mchango wa secta ya kilimo katika kuhamasisha Viwanda nchini , na zaidi ya washiriki zaidi ya miambili kutoka nchi mbalimbali mbali duniani watashiriki mkutano huo.
Aidha amesema kuwa mkutano huo pia unalenga katika kuongeza uelewa miongoni kwa watunga Sera kuhusu mchango wa kilimo katika kuhamasisha ukuajia wa Viwanda Tanzania , na washiriki pia watazungumzia kuhusu hatima ya wakulima wadogo na Masoko ya asili katika uchumi wa Viwanda kwa kuwa kilimo kina nafasi kubwa ya Kuongeza pato la Taifa

Post a Comment