WASLAM WATAKIWA KUSHEREHEKEA SIKUKUU KWA KUDUMISHA AMANI
Na John Luhende
mwambawahabari
Rais mstaafu wa jamuhuri ya mungano wa Tanzania Alhaji Ali Hassani Mwinyi anatarajiwa kuwaongoza waislamu katika siku ya kuzaliwa kwa kiongozi wa dini ya kiislaam mtume muhamad s.w alaih wasaal ifikapo disemba 11 maulidi ambayo kimkoa yatafanyika katika viwanja vya mnazi mmoja jijini dare s salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam sheikh mkuu wa mkoa wa dar es salaam ALHAD MUSSA SALUM amewaka waumini wa dini ya kiislamu kusherehekea mauli hayo kwa njia ya amani na usalama kama ilivyo amrishwa ya mtume muhamadi kwa waumini wake.
Amesema maulid hayo yataambatana na maandamano ya amani ambayo yatahamasisha suala la amani nchini yakifuatana na kauli mbiu isemayo muisalamu badilika amani na utulivu ndio maisha yetu.
Maulid ya kuzaliwa kwa mtume muhamadi kitaifa yatafanyika katika mkoa wa singida hivyo ametoa wito kwa waumini wote wa kiisalamu nchini kuungana na waislamu wote duniani kusherehekea na kuonesha heshima ya kuzaliwa kwa kiongozi huyo.
Post a Comment