Ads

JAFO ;WATUMISHI FANYENI KAZI ACHENI KUWAZA KUTUMBULIWA

Naibu waziri  wa nchi ofisi ya Rais TAMISEMI mh Suleiman Jafo wapili toka kushoto akizungumza na watumishi wa manispaa ya ilala ,aliyeko upande wa kukusto ni mstahiki meya wa Ilala Charles Kuyeko, na wapili kushoto ni katbu tawala wa mkoa DSM Teresia Mbando ,wakwanza kushoto ni mkurugenzi wa jiji la DSM Spora Liana picha na John Luhende.

Na.John Luhende 
mwambawahabari
Naibuwaziri wa nchi ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali  za mitaa  (TAMISEMI) Mh Suleiman Jafo amewataka watumishi wa waumma kufanya kazi kwa kujiamini  katika kutekeleza majukumu yao ili kuleta mabadiliko  ya  kimaendeleo katika Taifa.

Mh Jafo ameyasema hayo  leo wakati akizungumza na watumishi wa umma  wa manspaa ya Ilala na jiji la Dar es slaam  watendaji ,wabunge pamoja na madiwani  na kuwa elekeza wakuu wa idara kufanya kazi na kuwapa ushirikiano watumishi wangazi  za chini  katika idara zao na kuacha kuwanyanyasa .
Displaying JAFO ILALA WATUMISHI (27).jpg

‘’Nawaagiza wakuu wa idara  muache kuwa nyanyasa watumishi walio  chini yenu kwakuwa  wengi wanafanya kazi kwa hofu ya kuogopa kutumbuliwa  nakupelekea kutokuwa na amani katika maeneo yao ya kazi.’’ Alisema  Jafo

Aidha amesema  wizara yake itatoa ushirikiano kwa  watumishi wote wanaotekeleza majukumu yao kwa moyo na bidii na amewaagiza wakuu wa idara kuwa na utaratibu wa kutambua kazi za watumishi wanao jituma na kuvuka malengo ya kazi walio wekewa  hatakama hakuna pesa za kuwapa  angalau waandikiwe barua ama kupewa vyeti vya kutambua michango yao mahala pa kazi

Hata hivyo ame mpongeza  mkuu wa mkoa wa Dar es salaam , mkurugenzi wa jiji pamoja na madiwani  kwa kusimamia  suala  la usafi wa jiji kwakuwa kusimamia usasafi   japo kuna baadhi ya maeneo machache  ambayo bado ya naonekana  kulalamikiwa na wananchi

‘’Zamani jiji la Dar es salaam  lilikuwa chafu  lakinikwa sasa  hali imekuwa nzuri ukilinganisha na kabla ya kampeni ya usaf iliyo anzishwa na Rais  tarehe  9 Disemba  mwaka jana’’ alisema Jafo


Pamoja na hayo mh Jafo ameuagiza uongozi  wa manispaa ya ilala kwa kushirikiana na katbu tawala  mkoa wa  Dar es salaam  kupitia upya mkataba alio pewa mpangaji katika eneo lilo tolewa na Dawasco kwa ajili ya kujenga shule ya kata ya secondary  Buguruni   kutembelea eneo hilo na kisha kufanya maamuzi ili eneo hilo liweze kujengwa shule.

No comments