Ads

TRL YATANGAZA KUREJEA KWA HUDUMA ZA TREN KUANZIA DAR

mwambawahabariblog



Na John Luhende
mwambawahabariblog
Uongozi wa wa kampuni ya  Reli Tanzania  TRL  umetangaza  kurejea tena kwa huduma  zake za kusafirisha  abiria  na mizigo   kuanzia Dar es salaam  bada ya  kusitishwa kwa  huduma hizo  January  mwaka huu   kutokana   na  uharibifu  wa miundo mbinu  ya Reli ulisababishwa na mvua   kubwa  iliyo nyesha  maeneo ya  kilosa   mkoani    Morogoro na  Gulwe mkoni  Dodoma .

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini  Dar es salaam  kaimu meneja   mahusiano wa  kampuni hiyo  Mohamedi Mapondela huduma hizo  zina rejea mara baada ya matengenezo kukamilika  kwa jihihada kubwa  zilizofanywa  baina  ya  kampuni ya Reli na kampuni hozi ya  Reli RAHCO, ambapo matengenezo hayo yali anza January mosi   mwaka huu.


Aidha  ameishukuru serikali  pamoja na taasisi zake  kadhaa kwa  jitihada   zilizo fanikisha  kurejeshwa  kwa miundombinu  ya reli  na amewaomba radhi  wanachi walipata usumbufu kwa muda wote  wa matengenezo  kwa  safari   zilikuwa ziki ishia   Dodoma badala ya Dar  es salaam.


Amesema ,ratiba za  safari za treni ya kawaida  kutoka Dar es salaam kuelekea  Mwanza na kigoma  zita kuwa kila siku ya  jumanne na ijumaa saa11:00  jioni na  nazile za treni mpya  ya Delux, itakuwa ina ondoka Dar es salaam kila jumapili saa 2:00  asubuhi ,na kutoka  Mwanza na Kigoma  na treni ya kawaida  ina toka  huko kila siku ya Alhamis na Juma pili saa11:00  jion ,tren ya Delux nayo inatoka Mwanza na Kigoma  kila siku ya jumanne  saa2:00 asubuhi.

No comments