MultiChoice Africa yatangaza HAKUNA ONGEZEKO LA BEI kwa Wateja Wa DStv.

Umekuwa mwaka mgumu kwa
MultiChoice Africa. Masoko yetu yameathirika kutokana na kuporomoka kwa bei ya
bidhaa na mafuta na kushuka kwa thamani ya shilingi ya kitanzania. Gharama
nyingi za MultiChoice zipo katika dola ya Kimarekani kitu ambacho kilitulazimisha
kuongeza bei katika mwaka 2015.
Lakini hatupo peke yetu,
wateja wetu ambao ni rasilimali yetu kuu, wanateseka. Kwa hiyo tutafanya kitu
kidogo. Tumeamua kujitwisha sehemu ya mateso na hivyo HATUTAONGEZA bei kwa
wateja wa vifurushi vyote vya DStv kama ambavyo tumekuwa tukifanya kila mwezi
Aprili. Pasipo majanga mengine ya kiuchumi yasiyotarajiwa, hatutarajii ongezeko
la bei katika mwaka huu wa 2016.
Wateja ndio sababu ya
uwepo wetu, kwa hiyo tunadhamiria kuwaletea maudhui na vipindi bora kabisa kwa
bei nafuu. Tunataka muwe na wakati na uzoefu murua wa burudani za hapa nyumbani
na kimataifa katika televisheni.
Tuliianza safari mwezi
uliopita tulipozindua chaneli mpya za SuperSport ili kuwaletea Ligi Kuu Ya
Uingereza (EPL), Ligi Kuu ya Hispania(La Liga) na Michuano Ya Mataifa Ya Ulaya
(EURO 2016) kwa wateja wa kifurushi cha DStv Compact na hatuishii hapo. Mwezi
huu wa Aprili, chaneli za DStv zitaonyesha misimu mipya na kisasa kabisa ya
vipindi mfululizo ukiwemo msimu wa 6 unaosubiriwa kwa hamu wa Game Of
Thrones kuanzia kwenye M-Net Edge, Express kutoka US, sambamba na
telenovela mpya ya Hush ndani ya Africa Magic Showcase na The Voice:
Nigeria. Wateja pia wataburudishwa na chaguo za shoo mbalimbali za burudani
za ndani na kimataifa zinazopatikana katika vifurushi vya DStv ikiwemo
telenovela mpya ndani ya Zee World, East Meets West wakati marathoni ya
maudhui ya filamu “Wedding Season” ndani ya chaneli ya Universal itakonga mioyo
ya watazamaji kwa chaguzi kabambe za filamu za mapenzi na vichekesho. Marathoni
zaidi zinawasubiri ndani ya Studio Universal ambapo ‘Manscape’, ‘April Fools’,
‘Getting Away With it’ na marathoni za Steven Spielberg zitawaacha na vicheko
na msisimko.
Waigizaji wa Hollywood
wenye mvuto na wanaong’ara zaidi wataonyeshwa kupitia E! Entertainment huku #Richkids
Of Beverly Hills ikirudi na onyesho la kwanza la LA Clippers Dance Squad.
Jipatie kiti cha mbele kushuhudia nyota maarufu wanapopita katika zulia jekundu
katika maonyesho yaliyosheheni nyota wa uigizaji na burudani katika Black
Girls Rock 2016 ndani ya BET na 2016 MTV Movie Awards ndani ya MTV
Base. Mashabiki wa soka na wateja wa vifurushi vya DStv Premium, Compact Plus
na Compact pia watapatiwa burudani ya maonyesho ya moja kwa moja kutoka mechi
za Ligi Kuu Ya Uingereza (EPL), Ligi Kuu Ya Hispania (La Liga) na
michuano ya Kombe La Mataifa ya Ulaya 2016(Euro 2016) ndani ya SS3, SS11 na
SS12 huku upande wa Hispania wakijiandaa na mechi inayosubiriwa kwa hamu ya El
Classico kati ya Barcelona na Real Madrid tarehe 3 Aprili.
Kaimu Meneja Mkuu,
Francis Senguji amesema, “ Tunayo furaha kubwa kutangaza kwamba hakutokuwa
na ongezeko la bei katika vifurushi vyote vya DStv Aprili hii. Pasipo majanga
mengine ya kiuchumi yasiyotarajiwa, hatutarajii ongezeko la bei katika mwaka
huu wa 2016. Kwa maana hiyo mwezi ujao, wateja wa DStv watarajie
kuendelea kupata burudani za kuvutia kutoka DStv pasipo gharama zozote za
ziada”
Post a Comment