Ads

Tinga tinga kutafutiwa masoko nchini japani

Na Jesca Mathew
Mwambawahabariblog.
Kampuni  ya  kijapani ya Bricoleur Holdings Ltd imesaini mkataba wa miaka mitano na kikundi cha Sanaa ya uchoraji Tinga Tinga wenye lengo la kuwasaidia wasanii hao kuwatafutia masoko nchini japani na nchi za jirani .




Akizungumza na Waandishi wa habari Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Tanzania BASATA Godfrey Mngereza amesema kuwa fursa hiyo ni bora  na  itasaidia kukuza Sanaa ya uchoraji na kumfanya msanii kupata kipato na kuweza kuchangia pato la taifa kwa kuwa watakuwa na umiliki halali wa kazi zao.




Naye mwenyekiti wa chama hicho cha tinga tinga Zachi Zaburi ameishukuru kampuni hiyo kwani kupitia mkataba huo utaweza kuinua maisha yao kwa kujitangaza kwenye nchi mbalimbali kupitia uchoraji.


Katikati ni mwemyekiti wa tinga tinga Zuchi zuberi akionyesha mkataba huo kwa waandishi wa habari kushoto ni mkurugenzi wa  kampuni ya Bricouleur Ltd Bi Yu Shiran,kuliashoji Tsuchija mkurugenzi wa kampuni hiyo.




No comments