Ads

KUMBILAMOTO AIPONGEZA ZOLA KWA KAMPENI YA BUKUA USHINDE,AWATAKA WANANFUNZI KUACHANA NA MAKUNDI MABAYA.




Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akikabidhi madaftari kwa wanafunzi katika uzinduzi wa kampeni ya Bukua ushinde ya ZOLA ELECTRICT aliyepo upande wa kushoto  mwishoni ni mkurugenzi wa masoko wa  ZOLA ELECTRICT ndugu Eric Ballegu  aliyepo karinu na meya upande wa kushoto ni kaimu Afisa elimu sekondari Manispaa ya Ilala Rauri Temba  (Picha na Mwamba wa habari)




Baadhi ya wanafunzi waliofika katika uzinduzi wa kampeni ya Bukua ushinde iliyo andaliwa na ZOLA ELECTRIC

Na John Luhende 
Mwamba wa habari
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto , ameishukuru kampuni ya ZOLA inayojishughulisha na uuzaji wa  vifaa vifaa vya umeme jua kwa kushiriki katika kuhamasisha masuala ya Elimu kwa kuwazawadia wanafuznzi walio fanya vizuri katika mitihani  na kuwataka wananfunzi kujituma katika masomo.

Meya Kumbilamoto kayasema hayo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya bukua ushinde iliyoandaliwa na kampuni hiyo  amabapo amewataka wananfunzi hao kumshika Elimu wasi mwache aende zake.
"Jambo mlilolifanya ni jambo la kimungu maana tumeambiwa katika vitabu vitakatifu mshikeni elimu msimwache aeende zake ,ndugu zetu wa ZOLA  lengo lao ni kutokomeza ziro ,kadri muda unavyokwenda wataalamu wanastaafu wakuchuka hizo nafasi ni ninyi vijana chanamkeni katika masomo"Alisema 

Aidha Kumbilamoto amewataka wanafunzi hao  kutojihusisha na vitendo vya kihuni ikiwemo kuvuta bangi na kucheza kamali bali wautumie muda vizuri katika masomo.
"Kuna siku nilitembelea shule moja ya sekondari kuna wananfunzi walikuwa wanavuta bangi nakuombeni sana mjiepushe na vitendo hivyo na mjitume sana katika masomo  faida mtaiona mbeleni"Alisema 

Kwaupande wake Mkurugenzi wa Masoko wa ZOLA  ELECTRIC  Eliki Ballegu  amesema lengo la kuanzisha kampeni ya Bukua ushinde ni kusaidia na kuunga mkono juhudi za serikali katika kuinua kiwango cha elimu lengo lao ni kwenda kutoa hamasanchinzima  ila kwa sasa wameanza na mikoa minne Pwani Dar es salaam ,Arusha na Geita.

Mkurugenzi huyo amewataka wazazi  kumsihi mwanafunzi kutia nia ya kusoma na wananfunzi kutia jitihada ili weweze kujipatia zawadi kutoka ZOLA.

1 comment:

  1. Did you know there's a 12 word sentence you can say to your crush... that will trigger intense feelings of love and impulsive attractiveness to you deep inside his heart?

    Because deep inside these 12 words is a "secret signal" that fuels a man's instinct to love, worship and care for you with all his heart...

    12 Words Who Fuel A Man's Love Instinct

    This instinct is so hardwired into a man's genetics that it will make him try harder than ever before to take care of you.

    Matter of fact, fueling this mighty instinct is absolutely important to achieving the best ever relationship with your man that as soon as you send your man a "Secret Signal"...

    ...You will immediately find him expose his soul and mind for you in such a way he haven't experienced before and he'll perceive you as the one and only woman in the universe who has ever truly appealed to him.

    ReplyDelete