Ads

KATIBU TAWALA KIGAMBONI AGAWA HUNDI ZA MIKOPO YA AKINA MAMA,SOMA HAPA YAJAYO YANAFURAHISHA.




Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni Rahel Mhando, akigawa hundi kwa vikundi vya akinama wanaokpeshwa na Manispaa ya Kigamboni mikopo isiyo na riba jumla ya vikundi 25 leo vimepewa hundi .(Picha na John Luhende)


N a .John Luhende 
Mwamba wa habari
Halmashauri ya manispaa ya Kigambo leo imeanza kutoa Mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya akina mama, ambapo vikundi  23   vilivyo kidhi vigezo vimepatiwa mkopo wenye thamani ya shilingi million 45 bila riba.

Akizungumza kataika hafla ya kugawa hundi kwa vikundi hivyo vya akinamama Katibu tawala wa Wilaya ya Kigamboni Raheli Mhando  amevitaka vikundihivo  kuzitumiafedha hizo katika  kuendeleza biashara zao na kuzingatia muda wa kurejesha ili ili waweze kuongezewa zaidi.

‘’Wilaya yetu bado ni changa tutaendelea kuongeza fedha zaidi  kadiri ya uwezo wa Manispaa yetu, naomba mjitahidi kurejesha kwa wakati na mkikwama msikae kimya mje kutoa taarifa hatuwezi kuajakuuza vitu vyenu tutawaelewa tunaweza kuwaongezea muda Serikali yenu sikivu ina wajali‘’alisema

Aidha Mhando  amesema  pamoja na kuanza kutoa mikopo hiyo kwa akina mama,halmashauri inatoa mikopo kwa vijana na walevu ambapo  inaendelea kufanyiakazi taarifa za vikundi 18 vyavijana ambavyo vina tarajiwa kukopeshwa Pikipiki.

’’Waambieni huko na ndugu zetu walemavu waje kuchukua mikopo kwasasa idara inaendelea kufanyia kazi maelekezo ya mkuu wa Wilaya kwamba mikopo ya pikipiki itolewe kwa vikundi na siyo kwa mtu mmoja ikikamilika vija nao watapewa Pikipiki “ alisema

Naye  Afisa Maendeleo wa Manispaa ya Kigamboni Said Bakari , amesema Fedha hizo zitaendelea kutolewa kama serikali ilivyo agiza ,ambapo agizo la Serikali  ni kutoa asilimia kumi ya mapato kwa mgawanyo wa asilimia 4% vijana asilimia 4 %vijana na asilimia 2% kwa walemavu na sasa ni sheria na wataendelea kuitekeleza.

Kwaupande wao wanawake walipewa hudi hizo wameishukuru serikali ya awamu yatano kwa utaratibumzuri wa kuwakopesha lakini wameomba kiasi cha mkopo huo kiweze kuongezwa pindi wanapo kamilisha marejesho.

‘’Tuna shukuru Manispaa yetu kwa mikopo hii, itatusaidia sana sisi akinamama na biashara zetu  tutajitahidi kurejesha kwa wakati ili tupewe zaidi  na ninawaomba akimama wenzangu tujitahidi kurejesha .

“Alisema Sophia Mario mwenyekiti wa kikundi cha Milango saba  Vikoba Group.













No comments