MKUU WA WILAYA YA TEMEKE ASHIRIKI KUFANYA USAFI NA BENKI YA KCB
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaniva akishirikiana na wafanyakazi wa Benki wa KCB pamoja na wafanyabiashara wa eneo la Mbagara Zakiem wakifanya usafi katika eneo hilo mapema leo jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Wilaya
ya Temeke Mh. Felix Lyaniva ameiomba Benki ya KCB kutoa huduma nzuri na bora kwa wakazi wa Mbagara,
na ikiwezekana kuwapa punguzo la riba na masharti nafuu katika mikopo ili
kuweza kupata wateja wengi zaidi.
Ameyasema hayo
mapema leo jijini Dar es salaam wakati akifungua zoezi la usafi katika wilaya
hiyo lililofanywa na benki ya KCB maeneo ya Mbagara Zakiem, na kuwaomba punguzo
hilo kwa kuwa eneno hilo lina wafanyabiashara wengi wadogo na wanahitaji kupewa
nguvu ili waweze kufikia malengo yao.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mh. felix Lyaniva akiongea na wafanyabiashara pamoja na wafanyakazi wa KCB benki mapema leo jijini Dar es salaam.
Aliendelea kusema
kuwa anafurahia kuona wawekezaji wengi wanaendelea kuwekeza katika wilaya ya
Temeke kwani anategemea ubora wa huduma kwa wananchi wake, lakini pia
watamsaidia katika shughuli nyingi za kijamii ikiwemo kujenga Madarasa, Zahanati
na hata huduma za usafi katika maeneo hayo kwani ndio malengo ya serikali ya
awamu ya tano.
Mkuu wa
wilaya huyo aliendelea kusisitiza kuwa zoezi la usafi liwe ni endelevu kwani
yeye anafanya usafi kila jumaa mosi na sio mpaka iwe jumaa mosi ya mwisho wa
mwezi, lakini pia alisema anashukuru kupata wasaidizi kwani alikuwa akipata
usumbufu mkubwa hasa katika eneo hilo la Zakiem.
Meneja Masoko wa KCB Benki Christina Manyeye akitoa ufafauzi kwanini leo wameamua kufanya usafi katika eneo la Mbagara.
Kwa upande
wake Meneja Masoko wa KCB Benki Christina Manyeye alisema kuwa wameamua kufanya
zoezi hilo ili kuonyesha ushirikiano kati yao na wafanyabiashara pamoja na
wakazi wa maeneo hayo, japo kuwa ukiliangalia zoezi hilo kwa haraka haraka utaliona
kama ni dogo lakini kwao lina maana kubwa sana.
Aliendelea kusema
kuwa KCB Benki inaendelea kuwawezesha wafanya biashara wadogo wadogo katika
maeneo mbalimbali nje na ndani ya nchi, kama leo ilivyotoa zawadi za vitendea kazi kwa
wafanyabiashara wa eneo hilo kama miamvuli ya biashara na zawadi nyinginezo.
Na mwisho
alipenda kutoa shukrani za dhati wadau waliofanikisha zoezi hilo kwenda mbele
wakiwemo, Clouds Media Group, kampuni ya usafi ya West Pro, Creative Company,
Pamoja na kampuni ya Proper Media.



Post a Comment