ASANTE KOTOKO KUWASILI KESHO DAR KUMVAA MNYAMA SIMBA.
Kikosi cha Asante Kotoko kutoka Ghana kinawasili kesho jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kucheza na Simba Jumatano ya wiki hii.
Timu hiyo kongwe kutoka Ghana itawasili Jumanne tayari kukipiga na wekundu wa Msimbazi katika tamasha la Simba Day ambalo hufanyika kila mwaka inapofikia Agosti 8.
Kotoko ambao wapo nafasi ya 4 katika msimamo wa Ligi Kuu Ghana wakiwa na tofauti ya alama 3 dhidi ya Ashanti Gold iliyo kwenye nafasi ya kwanza huku kila timu ikicheza mechi 15, wamekubali mwaliko wa kuja nchini.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari Simba, Haji Manara, amesema Kotoko watakuja na kikosi chao kamili tayari kuwapa upinzani mkali Simba katika mechi hiyo.
Wakati Kotoko wakiwasili kesho, kikosi cha Simba kinawasili leo nchini baada ya kumaliza kambi ya wiki mbili ambayo walikuwa wameweka Instabul, Uturuki.
GOAL KEEPERS
-Felix Annan
Osei Kwame
DEFENDERS
-Amos Frimpong
-Samuel Frimpong
-Augustine Seha
-Wahab Adams
-Agyemang Badu
-Emanuel Owusu
-Awadu Nafiu
MILDFILDERS
-Akwasi Ntijk
-Jordan Opoku
-Prince Acquah
-Doglasuû Owusu
-Michael Yebouh
FORWADS
-Osman Ibrahim.
,-Obed Owusu
-Fedrick Boateng
-Sougne Yecoub
TECHINICAL TERM
-Paa Kwesi
-Akakpo Patron
-Ohene Brenya
-Nana Wasu
-Issa Amad
,- Sampson Apiah and
-Medical Term Officer
Yves Gyambimbi (Management)
Isaac Donkor ,( Management)
Obeng Seykere ( Ashanti Regional Circles Chairman)

Post a Comment