Ads

ALICHOKISEMA MBUNGE WA CUF, KUCHAUKA BAADA YA KUHAMIA CCM

Image result for zuberi kuchauka ccm

Mbunge wa jimbo la Liwale Mkoani Lindi kupitia chama cha wananchi Cuf Ndugu. Zuberi Kuchauka amerejea CCM ambapo aliondoka kwa muda mrefu tangu mwaka 2005 na kusema kuwa kurejea kwake kumetokana na Rais Magufuli kuirudisha misingi ya waasisi ambao ni TANU na ASP ambayo ilikosekana kwa muda mrefu ndani ya chama hicho.

Ameeleza kuwa sababu za kuondoka CUF ni kuwepo kwa mgogoro uliodumu kwa muda mrefu ndani ya chama hicho na kusababisha yeye kama kiongozi kushindwa kufanya kazi ya kuwaletea wananchi wake maendeleo na kushughulika na mgogoro kwa muda wote. 

Ameendelea kusema kuwa mkanganyiko uliopo ndani ya CUF umesababisha kuwa na makundi mawili ndani ya chama ambayo ni CUF ya Lipumba ambaye ni Mwenyekiti na CUF ya Maalim  Seif Katibu Mkuu wa chama hicho, na ukiwa katika kundi moja wapo kati ya hayo basi unaonekana msaliti kwa kundi lingine na ndio maana nimeamua kurejea CCM ili kuweza kuwatumikia wananchi.

Aliongezea kuwa toka Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani katika jimbo lake wamepata zaidi ya bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati mbili lakini pia serikali imepeleka  zaidi ya watumishi 80 ili kuboresha huduma jimboni humo.



No comments