JWTZ KESHO KUAGA MIILI YA MASHUJAA WETU WALIOUWAWA NCHINI DRC.
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linategemea kuaga Miili ya Mashujaa wetu waliouwawa wakiwa katika Jukumu la Ulinzi wa Amani nchini DRC hivi karibuni.
Marehemu wataagwa rasmi kesho Desemba 14, 2017 kuanzia saa 1 asubuhi katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Upanga jijini Dar es Salaam.
Wananchi wote wanakaribishwa katika kuaga Miili ya Mashujaa wetu.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Desemba 13, 2017.
Post a Comment