Ads

DIWANI MTARAWANJE AWAHAKIKISHIA WANANCHI WA KIJICHI KUWATUMIKIA KIKAMILIFU.

Mwambawahabari 
Diwani wa Kijichi, Eliasa Mtarawanje akilakiapo cha udiwani katika baraza la madiwani la Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Na Maria Kaira,Mwambawahabari
Diwani wa Kata ya Kijichi Eliasa Mtarawanje amewahakikishia wananchi wa kata hiyo kuwatumikia kikamilifu kwa kufata sheria na taratibu kwa lengo la kuwaletea maendeleo ndani ya kata hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuapishwa udiwani wake katika baraza la madiwani la Manispaa ya Temeke Mtarawanje ametoa wito kwa wananchi wa Kijichi kushirikiana katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo mbali mbali kwenye kaa hiyo.

“Napenda kuwashukuru wananchi wote wa kata yangu kwa kunichagua naomba tushirikiane katika kuleta maendeleo ya kata yetu mimi peke yangu sitoweza bila nyinyi”amesema


Mtarawanje amesema kuwa kijichi kunamiradi mbalimbali kilichobaki ni kuisimamia  vizuri ili wananchi waweze kupata huduma iliyo bora zitokana na miradi hiyo.



No comments