Ads

MBIVU NA MBICHI ZA UCHAGUZI JUMUIYA YA WAZAZI CCM DAR KUJULIKANA LEO


Mwambawahabari
Mjumbe wa Halmashauri  Kuu ya Chama cha Mapinduzi ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nani ya Nchi, Hamad Massauni amewapongeza madiwani waliofanya vizuri katika Uchaguzi mdogo wa Udiwani uliomalizika hivi karibuni katika baadhi ya mikoa.





Pongezi hizo amezitoa leo jijijini Dar es Salaam wakati akifungua Uchaguzi wa Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi wa chama hicho wa mkoa huo.

Amesema kutokana na sera madhubuti za CCM zlizotolewa kipindi cha kampeni kwa kiasi kikubwa zimechangia wananchi kushawishika kuwapigia kura wagombea waliofanikisha chama hicho kupata ushindi mnono.

“ Naomba niwapongeze viongozi waliomaliza muda katika nafasi mbalimbali pia kwa kile kipigo cha mbwa nawapongeza madiwani walioshiriki uchaguzi katika kata takribani 43,” amesema.

 Massauni amesema mshikamano na ushirikano ulionyeshwa na viongozi katika mchakato mzima uchaguzi umechangia chama hicho kupata ushindi wa kishindo.

Amesisisitiza kuwa  kutokana na utendaji madhubuti wa Serikali ya Awamu ya Tano ikiwemo kupambana na rushwa, ubadhirifu, matumizi mabayaya madaraka, matumzi mabaya ya rasilimali za umma huku akiongeza kuwa utendaji huo umesbababisha wapinzani kukosa ajenda.

Ameafafanua kuwa Rais John Magufuli ametekeleza ilani ya vyema ilani ya CCM na kwamba maalalmiko ya wananchi yaliyokuwa yakiwasilishwa Serikalini yamepungua ukilinganisha na kipindi cha nyuma.

Aidha, amesema chama hicho kilipoteza majimbo katika mkoa huo kutokana na baadhi ya wanachama wasaliti kukisaliti chama na kwamba wasaliti hao wameshaghulikiwa na ngazi husika.

Amewataka wagombea wanaoshiriki uchaguzi huo kuzitendea haki nafasi zao endapo watapata fursa ya kupigiwa kura  na wajumbe huku akibainisha nafasi wanazozigombea.

Kwa upande wake mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa wazazi wa jumuiya hiyo mkoani humo, Frank Kamugisha ,amesema  endapo atachaguliwa atakeleza vyema ilani ya chama pamoja na malengo ya kuwepo jumuiya hiyo.

Pia amesema chama hicho hakijawahi kushindwa katika jimbo lolote ila matokeo ya kushindwa husababishwa na mifarakano na migogoro baina ya wanachama.

Amewapaongeza wapinzani  waliojiunga na chama hicho kwani wameonyesha kujitambua na nia ya dhati kuiletea nchi maendeleo kwa kushirikiana na chama tawala.


No comments