Ads

WANASHERIA WA KUJITOLEA MKOA WA DAR ES SALAAM WAKABIDHI TAARIFA YA UTENDAJI KWA RC MAKONDA.



Na John Luhende  
mwambawahabari
Wanasheria wa kujitolea wa mkoa wa Dar es salaam walio itikia ombi la mkuu wa mkoa  wa Dar es salaam mhe, Paul Makonda kuwataka wanasheria kuwa saidia wananchi wa mkoa huo kuhusu mambo ya kisheria  leo wamekabidhi taarifa ya utendaji wa kazi hiyo kwa kipindi cha kuanzia 16/12/2016hadi 24/2/207.

Akiwasilisha taarifa hiyo kiongozi wa wanasheria  hao Geogia Kamina  amesema wamehudumia wananchi  10217  na jumla ya kesi  kesi 701  ziliweza kusikilizwa  ikiwemo migoro ya ardhi , kazi , mirathi na ndoa ,pamoja na kushugulikia migogoro sugu ilikaazaidi ya miaka kumi na sasa imekwisha , na kusema kuwa wanaishukuru serika kwa kuanzisha utaratibu huo kisheria .

Aidha Kamina  amefafanua kuwa  wanasheria hao waligawanyika  katika wilaya  zote za mkoa huo na walihudumu kwa makundi, wanasheria waliohudumia wilaya ya  Kigamboni walihudumia wananchi 29 na kusikiliza kesi 18, Ubungo walisikiliza  kesi 37  na kuhudumia wananchi ,806, Temeke walisikiliza kesi 200 nakuhudumia wananchi  20211, Kinondoni walisikiliza kesi 18 na kuhudumia wananchi776 , Ilala walisikiliza kesi 266 na walihudumia wananchi 3279 katika kipindi cha mwezi mmoja.

‘’Moja ya kesi ambayo ilitutia changamoto ni kesi ya mirathi ambayo faili la kesi hiyo lilipotea na shukurumungu tulifuatilia  hadi faili hilo lilipatikana   kesi hiyo ilidumu muda wa miaka kumi  na mama huyo mjane  alipatahaki yake’’ alisema mwanasheria Kamina
Ameongeza kuwa changamoto kubwa iliyopo ni wananchi wengi hawana uelewa kuhusu mambo ya kisheria  hivyo ndhahiri kuwa wanachi wanauhitaji  mkubwa wa msaada wakisheria.

Naye mkuu wa mkoa mko huo mhe. Paul Makonda  amewashukuru wanasheria hao na kuwa tia moyo kuwa kwa kazi hiyo kuwa imetia hamasa kwa wanasheria wengine na kuwataka wanasheria wengine kuiga mfano wa wanasheria hao kwa kufanya kazi za kujitolea kuisaidia jamii katika matatizo ya kisheria  ametoa rai kwa wana kwa wanasheria wa nkoa huu mwendelee kuwa saidia wanyonge akina mama na wote wasiojiweza katika kupata huduma za kisheria .

‘’Mji huu unawajanja wengi  na nchi yetu si wote tulibahatika kwenda shule wajanja hutumia fursa hiyo kuwa kandamiza wengine nawashukuru sana wanasheria  wote mlioshiriki katika kazi hii’’  alisema  Makonda 

No comments