KATIBU MKUU WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII ,MAJ.GEN MILANZI AWAONYA WAHITIMU WA MAFUNZO YA JESHI USU KWA WAHIFADHI WA WANYAMAPORI 103

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi akizungumza kwenye mkutano uliofanyika jana mjini Morogoro ulioandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori
Tanzania (TAWA) walipokutana na Wahifadhi Wakuu wa Mapori ya Akiba
nchini kwa lengo la kuweka mikakati ya kukabiliana na tatizo la
ujangili.
mwambawahabari
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi, amesema hatamvumilia mtumishi yeyote atayejihusisha na vitendo vya rushwa kuwa ni lazima ataondolewa mara moja ili asiendelee kuchafua taswira ya Wizara.
Alitoa rai hiyo jana wakati akifunga mafunzo ya jeshi Usu kwa wahifadhi wa
wanyamapori 103 kutoka Mamlaka ya Hifadhi Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori ( TAWA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ( NCAA).
wanyamapori 103 kutoka Mamlaka ya Hifadhi Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori ( TAWA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ( NCAA).
Alisema Wizara kwa sasa inabadili mfumo wa kiraia na kuendesha kwa mfumo wa kijeshi hivyo mtumishi yeyote asiyejihusisha na vitendo viovu vya namna yeyote Yule hatasalimika.
Wakati huo huo , Maj. Gen. Gaudence Milanzi alifungua mafunzo ya ukakamavu kwa maafisa wanyamapori wa daraja la pili kutoka
TAWA yatakayochukua muda wa wiki tano lengo likiwa ni kuwandaa
watumishi wa taasisi hiyo katika kuboresha mbinu za kupambana na majangili.

Akizungumza jana na wahitimu hao kabla ya kufunga mafunzo hayo katika kituo cha Mafunzo cha Mlele mkoani Katavi ,Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Milanzi aliwataka wahifadhihao wakaoneshe kile walichojifunza kwa kwa kujenga mahusiano mazuri na wanavijiji wanaozunguka hifadhi nchini baadala ya kujenga uadui.
Aliwasihi wahitimu hao kutumia silaha kwa weledi pale inapobidi hasa inapohitajika
kunusuru maisha ya watu na sio kuua.
kunusuru maisha ya watu na sio kuua.
Aidha,Milanzi aliwaagiza wakuu na viongozi wa taasisi zote zilizo chini ya Wizara wahakikishe wanashiriki katika mafunzo hayo kwa kuwa Wizara inatoka kwenye mfumo wa kiraia na kuelekea kwenye mfumo wa kijeshi katika utendaji wa shughuli za uhifadhi nchini.
Akitoa maelezo ya awali kabla ya hotuba ya Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii,
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TAWA, David Kanyatta aliwataka wahifadhi waliopewa mafunzo hayo wakajitume kwa kufanya kazi kwa bidii katika vituo vyao vya kazi ili kuonesha tija kwa taifa katika uhifadhi.

Kabla ya kuwahutubia wahitimu hao, Katibu Mkuu Milanzia alioneshwa mbinu mbalimbali kwa vitendo walizojifunza katika kupambana majangili ambao wamekuwa wakitumiasilaha nzito wakati wakifanya ujangili.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TAWA, David Kanyatta aliwataka wahifadhi waliopewa mafunzo hayo wakajitume kwa kufanya kazi kwa bidii katika vituo vyao vya kazi ili kuonesha tija kwa taifa katika uhifadhi.

Kabla ya kuwahutubia wahitimu hao, Katibu Mkuu Milanzia alioneshwa mbinu mbalimbali kwa vitendo walizojifunza katika kupambana majangili ambao wamekuwa wakitumiasilaha nzito wakati wakifanya ujangili.

Post a Comment