TANZANIA YAWA MFANO WA KUIGWA BARANI AFRIKA MRADI WA MABASI YA MWENDO HARAKA( DART)
Na JohnLuhende
mwambawahabari
Kutokana na Tanzania kufanikiwa katika sector ya usafitishaji hasa katika mradi wa Mabasi ya mwendo kasi DART ambao umeifanya kuwa nchi ya Tatu barani Afrika baadhi ya nchi za Afrika zimevitiwa na mradi huo na kuamua kuja kujifunza mafanikio ya mradi huo.
mwambawahabari
Kutokana na Tanzania kufanikiwa katika sector ya usafitishaji hasa katika mradi wa Mabasi ya mwendo kasi DART ambao umeifanya kuwa nchi ya Tatu barani Afrika baadhi ya nchi za Afrika zimevitiwa na mradi huo na kuamua kuja kujifunza mafanikio ya mradi huo.
Zimbabwe ni miongoni kwa nchi ambazo zime vutiwa na mradi huo , ambapo Waziri wa serikali za mitaa wa nchi hiyo Kasukuwere Savior amefanya ziara ya kutembelea mradi huo jijini Dar es salaam akiwa na Waziri wa serikali za mitaa (TAMISEMI).
Akizungumza na waandishi wa habari Waziri huyo amesema Zimbabwe imekumbwa na Changamoto ya usafiri ikiwemo foleni, amesema wanampango wa kuanzisha Huduma ya mabasi ya mwendo kasi (haraka) ili kupunguza msonga mano huo na kuchochea maendele na ukiaji uchumi , wameona Tanzania ndiyo nchi pekee wanapoweza kujifunza mbinu hizo.
Naye Waziri wa nchi ofisi ya Rais TAMISEMI mhe.George Simbachawene amewataka watanzania kujivunia mradi huo na kwamba Tanzania iko tayari kufanya ushirikiano na nchi zote zinazo hitaji kujifunza uta alam na mbinu mbalimbali za mradi huo .Mradi huo ulizinduliwa rasmi january 25 /2017 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. John Pombe Magufuli

Post a Comment