Ads

VIJANA ZAIDI YA ELFU TATU NCHINI KUFAIDIKA NA MRADI WA RED TO WORK


Badhi ya vijana waliojitokeza katika chuo cha usimamizi wa Fedha IFM,wakifanya usajiri kuingia katika mafunzo ya mradi wa Ready to work. 
Na ; Rayusa Yasini 
mwambawahabari
BANK ya Barcrays Tanzania kwa Kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la Junia Achievement wameanzisha mradi uitwao (Red to work) kwa Vijana zaidi ya elfu 3 waliopo vyuoni .

Akizungumza na Mwamba wa habari wakati wa zoezi la uendeshaji wa mradi huo katika chuo cha fedha (IFM) mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo Hamisi Kasongo amewataka Vijana kuchangamkia fursa hiyo pale watakapofika vyuoni mwao.

Amesema mafunzo ya red to work yatahusisha vyuo vya UDSM' IFM, TIA, CBE, UDOM, CHUO CHA KODI, MZUMBE , pamoja na MWALIMU NYERERE kwa ajili ya kupata ujuzi wa aina mbalimbali.


"Vijana wanatakiwa kutumia simu zao za mkononi kulog in program ya bank ya bacrays ili waweze kuingia online kwa urahisi kama watakavoelekezwa ili kupata fomu na kuweza kuijaza pamoja na kuanza mafunzo.

Ameongeza kuwa Vijana watakapo maliza mafunzo ya ujuzi wa kuweza kujiajiri, kutumia fedha zao vizuri, kulinda soko lake la ajira pale atakapojiajiri na kuajiriwa atakuwa mzalendo

Mafunzo hayo yataendesha kwa njia ya mtandao, kwa siku 90 ambapo mhitimu wa mafunzo hayo atatunikiwa cheti cha kimataifa kwa ushiriki wa mradi huo na ujuzi wa aina nyingi katika kulijenga taifa.


No comments