Ads

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA MAJALIWA ATAKA MABARAZA YA MADIWANI KUFANYA MAPITIO YA UPUNGUFU VYA VYUMBA VYA MADARAKA KATIKA HALMASHAURI NCHINI.


mwambawahabari
 Na Beatrice Lyimo
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa ametoa maagizo kwa  Mabaraza ya Madiwani nchini kufanya mapitio katika shule zote za Halmashauri ili kujua upungufu wa madarasa na kuanza mkakati wa utekelezaji wa  ujenzi wake.

Aliyasema hayo leo  wakati akipokea mchango wa madawati kwa shule ya msingi Chamazi kutoka Wizara Ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais la upatikanaji wa madawati katika shule za msingi na sekondari nchini.

Mhe. Majaliwa alisema  suala la upatikanaji wa madawati linakwenda sambamba na ujenzi wa madarasa hivyo ni wajibu wa kila halmashauri kuweka mkakati wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwani elimu bora ni pamoja na kuwa na mazingira rafiki ya kusomea.

‘Mbali na utekelezaji wa agizo la Rais juu ya mkakati wa upatikanaji wa madawati, suala hili linakwenda sambamba na ujenzi wa madarasa hivyo Serikali imeanza utekelezaji wa ujenzi huo  kwa maeneo machache hivyo ni jukumu la halmashauri kuhakikisha mnaandaa mikakati ya kuongeza vyumba vya madarasa’ alisema Majaliwa.

Aidha Waziri Mkuu Majaliwa alisema kuwa Serikali imeanza mkakati wa utekelezaji wa mpango wa  kutumia mfumo mpya wa upandishaji  madaraja walimu kwa kuwa  mfumo wa uliuotumika awali haukuwa na tija kwa maslahi ya walimu nchini.

Akipokea madawati hayo Waziri mkuu alisema kuwa anajua shida iliyopo ya upungufu wa madawati katika wilaya ya Temeke hivyo na kugawa madawati hayo katika shule tatu zilizopo katika Wilaya hiyo ikiwemo shule ya msingi Chamazi, shule ya msingi Mbande pamoja na shule ya msingi Majimatitu .

Kwa upande wake Waziri wa Wizara Ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi  Augustine Mahiga alisema  wizara yake ina jukumu la kuhakikisha inaitangaza nchi ili kuvutia wawekezaji na kukuza uchumi wa nchi, na kuongeza kuwa elimu bora ni msingi imara katika kufanikisha hilo.

Waziri Mahiga alisema Ubalozi wa Kuwait nchini pamoja na Jumuiya ya Mabohora wameikabidhi Serikali jumla 405 ili kuunga mkono jitihada za Rais ikiwemo
“Serikali ya Kuwait kupitia Ubalozi wake hapa nchini wametoa madawati  300 na kuahidi kutoa mengine 300 na Jumuiya ya Mabohora nao wamechangia madawati 105” alisema Balozi Mahiga.

Kwa mujibu wa Waziri Mahiga alisema watumishi wa Wizara yake walichanga kiasi cha Tsh. Milioni 100 ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha umma ili kuhamasisha umma kuhusu zoezi la upatikanaji wa madawati katika shule za msingi na Sekondari nchini.

No comments