WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA MAJALIWA ATAKA MABARAZA YA MADIWANI KUFANYA MAPITIO YA UPUNGUFU VYA VYUMBA VYA MADARAKA KATIKA HALMASHAURI NCHINI.
Na Beatrice Lyimo
WAZIRI Mkuu Kassim
Majaliwa Majaliwa ametoa maagizo kwa Mabaraza
ya Madiwani nchini kufanya mapitio katika shule zote za Halmashauri ili kujua
upungufu wa madarasa na kuanza mkakati wa utekelezaji wa ujenzi wake.
Aliyasema hayo leo wakati akipokea mchango wa madawati kwa shule
ya msingi Chamazi kutoka Wizara Ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ikiwa
ni utekelezaji wa agizo la Rais la upatikanaji wa madawati katika shule za
msingi na sekondari nchini.
Mhe. Majaliwa alisema
suala la upatikanaji wa madawati linakwenda
sambamba na ujenzi wa madarasa hivyo ni wajibu wa kila halmashauri kuweka mkakati
wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwani elimu bora ni pamoja na kuwa na
mazingira rafiki ya kusomea.
‘Mbali na utekelezaji
wa agizo la Rais juu ya mkakati wa upatikanaji wa madawati, suala hili
linakwenda sambamba na ujenzi wa madarasa hivyo Serikali imeanza utekelezaji wa
ujenzi huo kwa maeneo machache hivyo ni
jukumu la halmashauri kuhakikisha mnaandaa mikakati ya kuongeza vyumba vya
madarasa’ alisema Majaliwa.
Aidha Waziri Mkuu
Majaliwa alisema kuwa Serikali imeanza mkakati wa utekelezaji wa mpango wa kutumia mfumo mpya wa upandishaji madaraja walimu kwa kuwa mfumo wa uliuotumika awali haukuwa na tija kwa
maslahi ya walimu nchini.
Akipokea madawati hayo
Waziri mkuu alisema kuwa anajua shida iliyopo ya upungufu wa madawati katika
wilaya ya Temeke hivyo na kugawa madawati hayo katika shule tatu zilizopo
katika Wilaya hiyo ikiwemo shule ya msingi Chamazi, shule ya msingi Mbande
pamoja na shule ya msingi Majimatitu .
Kwa upande wake
Waziri wa Wizara Ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Augustine Mahiga alisema wizara yake ina jukumu la kuhakikisha
inaitangaza nchi ili kuvutia wawekezaji na kukuza uchumi wa nchi, na kuongeza
kuwa elimu bora ni msingi imara katika kufanikisha hilo.
Waziri Mahiga alisema
Ubalozi wa Kuwait nchini pamoja na Jumuiya ya Mabohora wameikabidhi Serikali
jumla 405 ili kuunga mkono jitihada za Rais ikiwemo
“Serikali ya Kuwait
kupitia Ubalozi wake hapa nchini wametoa madawati 300 na kuahidi kutoa mengine 300 na Jumuiya
ya Mabohora nao wamechangia madawati 105” alisema Balozi Mahiga.
Kwa mujibu wa Waziri
Mahiga alisema watumishi wa Wizara yake walichanga kiasi cha Tsh. Milioni 100
ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha umma ili kuhamasisha umma kuhusu zoezi la upatikanaji
wa madawati katika shule za msingi na Sekondari nchini.
Post a Comment