Ads

Wasanii nchini wahamasishwa kuchangamkia fursa ya sanaa inayodhaminiwa na British Council.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (kushoto) akiwasili katika Ofisi ya British Council Tanzania kwa ajili ya kuzindua Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.Kulia ni mwenyejji wake ambaye ni Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akiwahutubia wageni waalikwa pamoja na wanahabari kabla ya kuzindua Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.


Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge akiwahutubia wageni waalikwa pamoja na wanahabari wakati wa Uzinduzi wa Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.

Msanii wa kike toka Taasisi ya Culture and Development East Africa, Bi. Zuhura Seng'enge akiwapa burudani ya shairi wageni waalikwa pamoja na wanahabari wakati wa Uzinduzi wa Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.

Wasanii Gwakisa Mwambungu (kushoto) pamoja na Khalila Mbowe wakiwapa burudani ya nyimbo wageni waalikwa pamoja na wanahabari wakati wa Uzinduzi wa Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Masuala ya Sanaa Kenya na Afrika Mashariki toka British Council, Bi. Rocca Gutteridge akiwahutubia wageni waalikwa pamoja na wanahabari wakati wa Uzindua wa Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa, Bi. Leah Kihimbi akimkaribisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa ajjili ya kutoa hotuba kwa wageni waalikwa kabla ya kufanyika kwa Uzinduzi wa Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (kushoto) akizindua Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa, Bi. Leah Kihimbi, wa pili kulia ni Mkuu wa Masuala ya Sanaa Kenya na Afrika Mashariki toka British Council, Bi. Rocca Gutteridge na wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge.


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (kushoto) akiangalia bango lenye ujumbe kuhusu fursa ya sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa, Bi. Leah Kihimbi, wa pili kulia ni Mkuu wa Masuala ya Sanaa Kenya na Afrika Mashariki toka British Council, Bi. Rocca Gutteridge na wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akiimba huku akipiga gitaa mara baada ya kuzindua Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge.
 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akiwaonyesha Wageni waalikwa pamoja na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) picha aliyochorwa na mmoja wa Wasanii mara baada ya kuzindua Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (aliyevaa suti ya Kaunda) akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa British Council Tanzania pamoja na baadhi ya Viongozi wa Wizara mara baada ya Uzinduzi wa Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania 11 Julai, 2016 Jijini Dar es Salaam.
(Picha/Stori na Benedict Liwenga)
 
WASANII nchini wametakiwa kuchangamkia fursa ya kazi za sanaa ambayo inadhaminiwa na British Council Tanzania.

Wito huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye wakati wa Uzinduzi wa Fursa ya Sanaa kwa Tanzania na Afrika Mashariki ambayo Mdhamini wake ni British Council Tanzania.

Mhe. Nnauye amesema kuwa, uzinduzi wa fursa hiyo utawasaidia wasanii nchini, Mashirika mbalimbali yakiwemo Makampuni ya ndani ya Tanzania pamoja na Afrika Mashariki pamoja na Uingereza.

Amesema kuwa, fursa hiyo ni kubwa kwa wasanii nchini na kwa Taifa kwa ujumla, hivyo ameipongeza British Council Tanzania kwa kuja na wazo hilo zuri kwa manufaa ya wasanii nchini.

‘’Napenda nichukue nafasi hii kuwapongeza British Council Tanzania kwa kuwashirikisha wasanii na Makampuni mbalimbali na kuhakikisha kuwa fursa hizi zinamfikia kila msanii ndani ya Tanzania na kuwawezesha kushirikiana pamoja kwenye Sekta ya Sanaa na Utamaduni ndani ya Afrika Mashariki na Uingereza kwa ujumla’’, alisema, Mhe. Nnauye.

Ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara yake imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali ndani na nje ya Tanzania katika kuwawezesha wasanii katika kukuza vipaji vyao  na kupata fursa zinazowawezesha kuitangaza nchi yao.

‘’Serikali inatambua changamoto zinazowakabili wasanii wetu na imejikita katika kuhakikisha kuwa inatoa fursa zilizopo  kwa wasanii wetu’’.

Mhe. Nnauye amesema kuwa, Serikali itaendelea kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba inazidi kushirikiana na British Council Tanzania na wadau mbalimbali ili kukuza vipaji vya wasanii hao.

Kwa upande wake Mkuu wa Masuala ya Sanaa Kenya na Afrika Mashariki toka British Council, Bi. Rocca Gutteridge amesema kwamba, fursa inayodhaminiwa na British Council inalenga kuwawezesha Wasanii wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kuwa karibu kwa kushirikiana katika vipaji vyao na hivyo wameanzisha na platfomu maalum ambayo wasanii hao watakuwa wakisaidiana katika kazi zao.

Naye Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge amesema kuwa katika kuanzishwa wa fursa hiyo, kutakuwa na Miradi kati ya mitatu hadi tano ambayo itachaguliwa katika mwaka wa 2016/17  ambapo kila mradi utapewa fedha kiasi cha Euro elfu 20.

Ameongeza kuwa, British Council inalenga kusaidia zaidi ya wasanii 60 wa Afrika Mashariki ambapo wataweza kusafiri ndani ya Afrika Mashariki kwa kipindi cha miezi tisa ijayo.

No comments