Ads

SIMBA ULIMINJE KWA AZAM, YAPATA USHINDI KWA MBINDE

Vinara wa ligi kuu soka Tanzania Bara klabu ya Simba imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam FC.

Ushindi huo wa Simba unaifanya Azam FC kubaki katika nafasi ya tatu ikiwa na alama 33 ikiachwa rasmi na Yanga yenye alama 34 katika nafasi ya pili.

Bao pekee lililoipa ushindi Simba limefungwa na nyota Emmanuel Okwi dakika ya 36 na kumfanya mshambuliaji huyo raia wa Uganda kufikisha mabao 13 akiwa juu ya washambuliaji Obrey Chirwa mwenye mabao 10 na John Bocco tisa.

Ushindi wa leo umeifanya Simba ijiongezee alama tatu na kufikisha alama 41 kileleni ikiziacha Yanga yenye alama 34 katika nafasi ya pili na Azam FC yenye alama 33 katika nafas ya tatu

No comments