Ads

RAIS Dkt Magufuli akutana na Maafisa Wakuu sita wa JWTZ wanaotarajiwa kustaafu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo kabla hajaanza kuwatambulisha Maafisa Wakuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (hawaonekani pichani) ambao wanatarajia kustaafu. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo ambaye aliambatana na Maafisa Wakuu (sita)  wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ambao wanatarajiwa kustaafu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo pamoja na Maafisa Wakuu (sita) wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania  wanaotarajiwa kustaafu ambao ni Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania Luteni Jenerali James Mwakibolwa wanne kutoka (kulia), Meja Jenerali Michael Isamuhyo watatu kutoka (kulia) Brigedia Jenerali Aron Robert Lukyaa wapili kutoka (kulia), Kanali Peter Samuel Sameji wa kwanza (kulia).  Wengine katika picha ni Brigedia Jenerali William Ephraim Kivuyo wapili kutoka kushoto na Brigedia Jenerali Elizaphani Lutende Marembo. PICHA NA IKULU

No comments