Mstahiki Meya Dodoma “tuenzi Mashujaa kwa kufanyakazi” Na. Immaculate Makilika
Na Beatrice Lyimo
Mwambawahabari
WASANII wa Filamu nchini wanatarajia kunufaika na kazi zao kufutia makubiliano ya Kampuni ya Star Media Tanzania Ltd (Startimes), pamoja na Steps Entertainment za kutumia kazi zao kwenye vituo vya televisheni nchini.
Akizungumza waandishi wa habari leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Sibuka Media, Dkt. George Nangale alisema kazi hiyo itafanywa kwa ushirikiano na taasisi hizo ili kuweza kuwasaidia wasanii kunufaika na kazi zao kupitia luninga badala ya kuwasubiri wateja wao kuzinunua katika santuri (DvD).
“Tumefikia uamuzi huu baada ya kuona ombwe lililopo sasa katika kuzifikisha filamu zetu kwa walio wengi pamoja na kwamba Watanzania wana mwamko mkubwa wa kuzitazama filamu hizi zenye mafunzo ya maisha na burudani” alisisitiza Mkurugenzi huyo.
Kwa upande wake Msanii wa Bongo Movie, Mwanaheri Hamad alisema uonyeshaji wa kazi zao katika vituo vya televisheni utawanufaisha wasanii chipukizi ambao kazi zao bado hazijaonekana.
Amesema kuwa kutokana na mkataba huo wa kurusha filamu hzo umerahisisha soko za kazi hizo katika mfumo DvD ambapo ulikuwa unatumiwa hapo awali.
Filamu hizo zitaonyeshwa kupitia king’amuzi cha StarTimes chaneli 111 ikijulikana kama Sibuka Maisha Steps chaneli kila siku na itaanza kuonyeshwa Ijumaa hii tarehe 29 Julai, 2016.
Post a Comment